Dar es Salaam:: Mahindi TSH:39-45000 per 100kg || Maharage TSH:80-120000 per 100kg|| Mchele TSH:93-120000 per 100kg|| Mtama TSH:45-50000 per 100kg||Ngano THS:61-70000 per 100kg|| Ulezi TSH:55-65000 per 100kg|| Uwele TSH:35-40000 per 100kg|| Viazi mviringo TSH:38-50000 per 100kg|| Source: Wizara ya Viwanda na Biashara
Mwanzo arrow Kuhusu Sisi
kuhusu sisi PDF Print E-mail

Asasi ya Maendeleo ya Vijana [Tanzania Development Forum for Youth] ni taasisi isiyokuwa ya kiserikali, isiyofanya shughuli zake kwa faida, isiyofungamana na chama chochote cha kisiasa, na ni taasisi inayongozwa na vijana.

Asasi ya maendeleo ya vijana imeanzishwa mwaka wa 2005 na kusajiliwa Februari mwaka wa 2006 chini ya sheria ya taasisi zisizokuwa za kiserikali ya mwaka 2002 ikiwa na namba ya usajili No.00NGO/0643.

Kama taasisi iliyosajiliwa, Asasi ya Maendeleo ya Vijana imepewa mamlaka ya kufanya kazi katika taasisi zisizokuwa za kiserikali ikiwa na madhumini ya kuendeleza vipaji na kuwawezesha vijana kutumia fursa mabalimbali ambazo zimewazunguka kupitia uelimishaji rika pamoja na mafunzo mbalimbali.

Asasi ya maendeleo ya vijana inafanya kazi katika ngazi ya kitaifa. Asasi ya maendeleo ya vijana ina malengo manne ikiwa ni pamoja na kuwaletea vijana maendeleo na demokrasia kwa;

  • Kuwawezesha vijana kushiriki katika shughuli mbalimbali za kilimo na biashara.
  • Kuchangia katika kusuluhisha migogoro mabalimbali kati ya wakulima na wafugaji
  • Kuwapatia vijana elimu ya uraia
  • Kuwaelimisha vijana kuhusu ugonjwa wa UKIMWI tukiwa na kipao mbele kwa vijana katika jamii za kifugaji